Unisciti a noi in un viaggio nel mondo dei libri!
Aggiungi questo libro allo scaffale
Grey
Scrivi un nuovo commento Default profile 50px
Grey
Iscriviti per leggere l'intero libro o leggi le prime pagine gratuitamente!
All characters reduced
Hadithi Yako ya Kweli - Mwongozo Muhimu wa Siku 50 Kwa Ajili ya Maisha Yako Mapya Pamoja na Yesu - cover

Hadithi Yako ya Kweli - Mwongozo Muhimu wa Siku 50 Kwa Ajili ya Maisha Yako Mapya Pamoja na Yesu

Susan Freese

Traduttore Christian Lingua

Casa editrice: Publishdrive

  • 0
  • 0
  • 0

Sinossi

JINUNULIE KIMOJA. MNUNULIE MTU KIMOJA KAMA ZAWADI.* Maisha yako yanaweza kubadilika ndani ya Siku 50. Zana hii KAMILI ya Kujifunza Biblia ina mambo muhimu juu ya uanafunzi kwa ajili ya Wakristo wapya ulimwenguni kote (hakuna mifano ya kimagharibi). Ni vigumu kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu na kutimiza kusudi lako bila ufahamu mzuri wa hadithi Yake na sehemu yako katika hadithi hiyo.
 
Masomo haya 50 ya kila siku yanafunua MAMBO MUHIMU YA IMANI ili kufanya urafiki wako na Yesu uwe wa kina na kukupa UJUZI WA KIUTENDAJI ili iwe mfuasi Wake.
 
Jifunze kile ambacho waumini wakomavu wamejua kwa miaka mingi ndani ya Siku 50 kupitia safari hii rahisi lakini inayobadilisha maisha.
 
Wiki ya 1:    Hadithi ya Mungu—Kugundua hadithi kuu ya Biblia
 
Wiki ya 2:    Hadithi Yako—Kukumbatia utambulisho wako mpya katika Kristo
 
Wiki ya 3:    Kusudi Lako—Kutimiza kusudi la maisha yako
 
Wiki ya 4:    Kukaa Ndani—Kubaki Ukiwa Umeunganishwa  na Mungu
 
Wiki ya 5:    Neno la Mungu—Kumsikiliza Mwanzilishi wa Uzima
 
Wiki ya 6:    Neno la Mungu—Kunena na Mwanzilishi wa Uzima
 
Wiki ya 7:    Roho Mtakatifu—Kutimiza Hadithi Yako Kwa Nguvu Za Mungu
 
Kila wiki utajifunza zaidi juu ya simulizi ya Biblia.
 
Utagundua siri za maisha ya Kikristo, kama vile jinsi ya kukaa ndani ya Kristo, kushughulikia shaka, kupinga majaribu, na kumwabudu Mungu katika misimu ya mateso.
 
Pia utajifunza njia za kiutendaji za kujifunza Biblia yako, kushiriki imani yako, kufanya wanafunzi, na kuomba. Ikiwa hujaanzisha uhusiano na Yesu, utapata fursa ya kuchukua hatua hiyo.
 
Kila siku inatamatishwa kwa mbinu ya Amri Kuu ya kutumia Maandiko, maswali, maombi, na mahali pa kuchukua hatua zako zinazofuata.
 
KITABU HIKI NI KWA AJILI YAKO IKIWA:
 
- Wewe ni muumini mpya katika Yesu unayetafuta hatua zinazofuata za kukuza imani yako,
 
- Wewe ni Mkristo anayetafuta kufundishwa kuwa mwanafunzi au kuwafundisha wengine kuwa wanafunzi,
 
- Unachunguza Ukristo na unataka kujua jinsi ya kuwa mfuasi wa Yesu.
 
MAISHA YAKO YANA HADITHI MPYA YA KUSIMULIA:
 
Shuhudia imani ya kweli na furaha unapotumia kweli takatifu kubadilisha maisha yako. Kukutana na Yesu ni mwanzo tu. Kumfuata--hivyo ndivyo hadithi yako ya kweli inavyojitokeza.
 
--Maneno muhimu, maswali ya kutafakari ya kibinafsi ya kila siku na ya majadiliano ya kikundi ya kila wiki yamejumuishwa.
 
-- Kimeandikwa kwa ajili ya wasomaji kutoka kote duniani bila mifano ya kimagharibi.
 
--Zaidi ya saa 10,000 za utafiti, hakiki 3 za kitheolojia, marejeo zaidi ya 1,400 ya kibiblia, wasomaji zaidi ya 50 wa kutoa maoni ya awali = Safari 1 Inayobadilisha Maisha.
 
Taarifa zaidi zinapatikana kwenye yourtruestorybook.com
 
Mapato kutoka kwa kila kitabu kinachouzwa yatatoa nakala iliyotafsiriwa kwa muumini ambaye hana nyenzo za kutosha katika nchi inayoendelea.
Disponibile da: 19/01/2024.
Lunghezza di stampa: 368 pagine.

Altri libri che potrebbero interessarti

  • KITABU CHA HENOKO - The Book of Enoch in Swahili - cover

    KITABU CHA HENOKO - The Book of...

    Mwami

    • 1
    • 1
    • 0
    Henoko akajibu, akasema, Mimi, Henoko, mwenye haki, ambaye macho yake yalifunguliwa na Mungu, ili nipate kuona maono ya Yeye Aliye Mtakatifu mbinguni, ambayo malaika walinionyesha; na kutoka kwao nikasikia kila kitu, nikaelewa Niliona, lakini si kwa kizazi hiki, lakini kwa ajili ya vizazi vya mbali ambavyo vinakuja. Kwa habari ya wateule nilisema, nikatoa mfano juu yao: Mtakatifu, na Mkuu atatoka katika makao yake, Mungu wa ulimwengu. Akitoka huko ataukanyaga mlima Sinai, na kuonekana pamoja na majeshi yake, na kwa nguvu za uweza wake ataonekana kutoka mbinguni. Kila mtu atapigwa na hofu, na walinzi watatetemeka, na hofu kuu na tetemeko litawashika hata miisho ya dunia. Milima mirefu itatikisika, na vilima virefu vitashushwa, na kuyeyuka kama nta mbele ya mwali wa moto. Dunia itapasuka, na vyote vilivyo juu ya nchi vitaangamia, na kutakuwa na hukumu juu ya kila kitu, na juu ya wote wenye haki. Lakini kwa wenye haki atawapa amani, na kuwalinda wateule, na neema itakuwa juu yao, na wote watakuwa wa Mungu, na itakuwa vizuri kwao, na watabarikiwa, na nuru ya Mungu. itawaangazia. Hakika! Anakuja na maelfu ya watakatifu wake ili kutekeleza hukumu juu yao, naye atawaangamiza waovu, na atawahukumu wote wenye mwili na hatia kwa ajili ya mambo yote ambayo wenye dhambi na wasiomcha Mungu wametenda dhidi yake.
    Mostra libro
  • japji kiswahili kutafakari - safari kwa roho - cover

    japji kiswahili kutafakari -...

    Thaminder Thamindersinghanand

    • 0
    • 0
    • 0
    1.safari kwa roho 
    2.Safari ya kuelekea Kiroho 
    Guru Granth Sahib ni Guru aliye hai wa milele, muundo wa kishairi wa Sikh Gurus, Watakatifu wa Kihindu na Waislamu. Mkusanyiko huo ni zawadi kutoka kwa Mungu kupitia kwao kwa wanadamu wote. Maono katika Guru Granth Sahib ni ya jamii yenye msingi wa haki ya Kimungu bila ukandamizaji wa aina yoyote. Ingawa Granth inakubali na kuheshimu maandiko ya Uhindu na Uislamu, haimaanishi upatanisho wa maadili na mojawapo ya dini hizi. Katika Guru Granth Sahib wanawake wanaheshimiwa sana na majukumu sawa kama wanaume. 
    Wanawake wana roho sawa na wanaume na hivyo wana haki sawa ya kukuza hali yao ya kiroho na nafasi sawa ya kupata ukombozi. Wanawake wanaweza kushiriki katika shughuli zote za kidini, kitamaduni, kijamii, na kidunia ikiwa ni pamoja na kuongoza makutano ya kidini. Sikhism inatetea usawa, haki ya kijamii, huduma kwa ubinadamu, na uvumilivu kwa dini zingine. Ujumbe muhimu wa Kalasinga ni ibada ya kiroho na uchaji wa Mungu wakati wote wakati wa kutekeleza maadili ya huruma, uaminifu, unyenyekevu na ukarimu katika maisha ya kila siku. Kanuni tatu za msingi za dini ya Sikh ni kutafakari na kumkumbuka Mungu, Kufanya Kazi kwa ajili ya kuishi kwa Uaminifu na kushiriki na wengine.
    Mostra libro
  • Here comes A Day of Darkness - SWAHILI EDITION - School of the Holy Spirit Series 9 of 12 Stage 1 of 3 - cover

    Here comes A Day of Darkness -...

    Lambert Okafor

    • 0
    • 0
    • 0
    Inakuja Siku ya Giza
    
    Kila kitu sio sawa na sayari. Dunia!
    Matukio yasiyo ya kawaida yanayotokea sasa ulimwenguni kote ni ishara fasaha - kwa wale ambao wangeyatii.
    Wanasayansi - wa zamani na wa kisasa - wote wanakubali kwamba kitu cha kutisha kinapaswa kutokea, na kwamba mwanadamu hana wakati mwingi uliobaki. Ulimwengu unaweza kufikia mwisho hivi karibuni - walisema. Kipindi wanachokielekeza bila shaka kitamtisha mtu yeyote.
    Ripoti za anga kutoka kwa satelaiti zenye nguvu nyingi na kompyuta za hali ya juu, zote zinathibitisha ukweli huu mbaya! Siku mbaya zimefika mwishowe.
    Kutoweka kwa tabaka la ozoni, kuongezeka kwa mawimbi ya joto, mabadiliko ya hali ya hewa...mawimbi makubwa ya maji na mafuriko yanayoharibu viwango visivyo na kifani, matetemeko ya ardhi yanayoongezeka na uharibifu wa mazingira unaozidi kuwa mbaya duniani - hizi ni dalili za hatua ya mwisho!
    NA HIVYO, MUNGU KATIKA UPENDO WAKE AMEONGEA TENA KUHUSU YALE YANAYOJIRI KUTOKEA...
    Tafadhali soma Ujumbe huu wa Ufunuo usio wa kawaida na uchukue hatua haraka kabla haujafikia ‘digrii- 46’.
    * Yeyote anayependa sayansi lakini anadhihaki Injili anapaswa
    upesi fungua Sura ya Tatu ya kitabu hiki—kwa jambo la kushangaza!
    * Pia, yeyote anayehusika na kazi ya Injili anapaswa kurejelea Sura ya Tano - kwa HABARI fulani za KUSIKITISHA!
    Mostra libro
  • The Coming WORLD RELIGION and the MYSTERY BABYLON - SWAHILI EDITION - School of the Holy Spirit Series 11 of 12 Stage 1 of 3 - cover

    The Coming WORLD RELIGION and...

    Lambert Okafor

    • 0
    • 0
    • 0
    DINI YA ULIMWENGU Inayokuja na BABELI YA SIRI
    
    Moja ya unabii wa kutisha sana wa wakati wa mwisho unakaribia kutimizwa, yaani, unabii kuhusu DINI YA ULIMWENGU MMOJA - wakati dini zote na madhehebu mbalimbali yatakusanyika kutekeleza ibada ya Kishetani ya ulimwengu mzima!
    
    Wakati huo, waamini wa kweli katika Kristo watakuwa katika hatari kubwa kupitia mateso ambayo hayajawahi kutokea ambayo yatatekelezwa na mataifa yote ya dunia (Mathayo 24:9). Saa hiyo pia upendo wa Wakristo wengi utapoa kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kumpinga Kristo (Mathayo 24:12). Hata hivyo, wale walio na maarifa na walioandaliwa mapema watashinda (Danieli 11:32).
    
    Waumini wanapaswa kujiandaa vipi? Mambo haya ni ya dharura!.. .Maana ile Siri ya Uasi tayari inatenda kazi... (2Wathesalonike2:7).
    Mostra libro
  • How To Hear From God - SWAHILI EDITION - School of the Holy Spirit Series 7 of 12 Stage 1 of 3 - cover

    How To Hear From God - SWAHILI...

    Lambert Okafor

    • 0
    • 0
    • 0
    NAMNA YA KUSIKIA KUTOKA KWA MUNGU
    Niliandika kijitabu hiki kwa sababu ya maswali mengi niliyopokea kutoka kwa waamini, wengine kupitia barua na wengine kupitia ziara za kibinafsi, yote yakihusu jinsi ya kusikia kutoka kwa Mungu! Nilishangaa mara ya kwanza wakati baadhi ya maswali yalipotoka kwa watu niliowaona kuwa Wakristo waliokomaa sana. Punde, niligundua kwamba hili lilikuwa tatizo moja ambalo kwa hakika lilikumba kada zote za waumini, lakini tatizo moja ambalo lilizingatiwa mara chache sana katika makanisa yetu mbalimbali!
    Si ajabu watu wanaona ni rahisi kusema, “mchungaji wangu alisema…”, badala ya “Bwana alisema”! Na kwa hivyo, wakati mchungaji anapoteleza, kila mmoja pia anajitenga naye, kwa sababu hakuna anayeweza kufanya uchunguzi wa kujitegemea moja kwa moja kutoka kwa Bwana. Hiyo ni sawa na Waisraeli kule Jangwani ambao waliweza tu kusikia na kumnukuu Musa, lakini hawakuthubutu kuingiliana na Mungu wao moja kwa moja. Katika mchakato huo, wote waliangamia kwa kuwa hawakujua njia za Mungu! Ni jambo la hatari kama nini wakati huu wa mwisho kwa mwamini yeyote kumtegemea kabisa mchungaji!
    Iliuumiza moyo wangu zaidi nilipogundua kwamba Bwana alikuwa akizungumza na wengi wa watu hawa, tu kwamba, kama Samweli, hawakuweza kutambua sauti yake. Walichohitaji tu ni mtu wa kuwaelekeza, kama vile Eli alivyomfanyia Samweli. Na akina Eli wa wakati wetu wanaonekana kuwa na shughuli nyingi sana na masuala mengine.
    Ikiwa wewe ni mmoja wa wale ambao wamekuwa wakiteseka kimya kwa muda mrefu juu ya suala hili la kusikia kutoka kwa Baba yako wa Mbinguni, unapaswa sasa kufurahi kwa kuwa hitaji lako litatimizwa hivi karibuni, na Bwana Mwenyewe, kupitia mikataba hii ndogo.
    
    Bwana Yesu akubariki sana unaposoma. Amina.
    
    Lambert .E. Okafor
    Mostra libro
  • Mwongozi Wa Roho - Safari Maishani - cover

    Mwongozi Wa Roho - Safari Maishani

    Ken Luball

    • 0
    • 0
    • 0
    ”Nini Maana ya Maisha”?Mwongozi wa RohoPUBLISHER: TEKTIME
    Mostra libro